Ofisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Pemba.
Ofisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Pemba imeanzishwa kwa lengo la kusimamia na kuratibu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi katika Kisiwa cha Pemba. Ofisi hii inahakikisha kuwa usimamizi wa nyaraka na kumbukumbu unafanyika kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za kitaalamu, pamoja na kurahisisha upatikanaji wa huduma za nyaraka kwa wananchi na watafiti waliopo Pemba. Ofisi hii inaongozwa na Mratibu
Ofisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Pemba inaendelea kuimarisha juhudi za kulinda na kuhifadhi kumbukumbu muhimu za kihistoria pamoja na kuboresha huduma za nyaraka katika Kisiwa cha Pemba.
Majukumu
Majukumu ya Ofisi ya Nyaraka na Kumbukumbu Pemba ni pamoja na :-
- Lengo kuu la Ofisi ya Pemba ni kusimamia, kulinda na kuhifadhi nyaraka na kumbukumbu kwa matumizi ya Serikali na jamii kwa ujumla katika Mkoa wa Pemba.
- Kusimamia utekelezaji wa mifumo bora ya utunzaji na uhifadhi wa nyaraka na kumbukumbu katika taasisi za umma zilizopo Pemba
- Kusimamia miongozo na ushauri juu ya uchambuzi wa nyaraka zisizo na thamani ya kudumu ili ziweze kuteketezwa kwa kufuata taratibu rasmi
- Kuratibu na kusimamia zoezi la uhamishaji wa nyaraka na kumbukumbu zenye thamani ya kudumu kwenda katika vituo rasmi vya uhifadhi vilivyopo Pemba
- Kufanya ukarabati na uhifadhi (restoration na conservation) wa nyaraka muhimu zilizoharibika au zilizo katika hatari ya kupotea
- Kutoa huduma za utafiti, rejea na ushauri kwa watafiti, wanafunzi na wananchi kuhusu nyaraka zilizohifadhiwa katika vituo vya Pemba
- Kushirikiana na Ofisi Kuu Unguja katika kuimarisha sera, miongozo na mipango ya maendeleo ya sekta ya nyaraka na kumbukumbu